Monday, December 31, 2018

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LAKABIDHI MASHINE ZA KUFYATULIA TOFALI KWA JESHI LA MAGEREZA

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na huduma kwa jamii Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Yahya Charahani (mwenye shati jeusi) akikabidhi mashine za kufyatulia tofali kwa Afande Hassan Lindenge wa Jeshi la Magereza na Afande Lwesya wakati wa kukabidhi mashine za kuengenezea matofali ya kisasa yanayoendana na hali ya udongo na miamba ya eneo husika. Mashine hizo zitatumika na Jeshi la Magereza kufyatua matofali yatakayotumika katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya jengo hilo.

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limekabidhi mashine za kisasa za kufyatua matofali kwaajili ya kusaidia kusukuma mbele shughuli mbalimbali za ujenzi za jeshi la Magereza  nchini.
Mashine hizo zilikabidhiwa kwa Kamanda Hassan Lindege wa Bohari Kuu ya Magereza kwenye ofisi za NHC Temeke kwenye hafla fupi na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na huduma kwa jamii Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Yahya Charahani.
Katika hafla hiyo Kamanda Lindenge alilishukuru Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuwezesha utoaji wa mashine hizo kwani zitasaidia kwenye shughuli mbalimbali za ujenzi wa jeshi hilo na akaahidi kupeleka wataalamu wa jeshi hilo kwenye mafunzo ya ufyatuaji tofali kwa taasisi ya NHBRA.
Akikabidhi Mashine hizo Charahani kwa Kamanda Lindenge alisema mashine hizo zitawasaidia Jeshi la Magereza kujenga nyumba za gharama nafuu kwa kutumia matofali yanayoingiliana bila kutumia udongo yatakayofyatuliwa kwa kutumia mashine hizo za kisasa.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Kaimu Meneja wa NHC Temeke, Injinia Renald Kazoba alisema mashine hizo ambazo ni bora kabisa za gharama nafuu zikitumika vyema zitaweza kuwazalishia Jeshi la Magereza matofali mengi sana na hivyo kuwapunguzia gharama za ujenzi na kuongeza ubora wa kazi.

 Kaimu Meneja wa NHC Temeke, Injinia Renald Kazoba akionyesha namna mashine hizo zinavyofanya kazi.
 Kaimu Meneja wa NHC Temeke, Injinia Renald Kazoba akitoa maelezo ya  namna mashine hizo zinavyofanya kazi.

 Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na huduma kwa jamii Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Yahya Charahani(mwenye shati jeusi) akikabidhi mashine za kufyatulia tofali kwa Afande Hassan Lindenge wa Jeshi la Magereza wakati wa kukabidhi mashine za kuengenezea matofali ya kisasa yanayoendana na hali ya udongo na miamba ya eneo husika. Mashine hizo zitatumika na Jeshi la Magereza kufyatua matofali yatakayotumika katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya jengo hilo.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na huduma kwa jamii Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Yahya Charahani (wa pili kulia) wakati wa kukabidhi mashine za kuengenezea matofali ya kisasa yanayoendana na hali ya udongo na miamba ya eneo husika. Wanaosikiliza ni Kaimu Meneja wa NHC Temeke, Injinia Renald Kazoba na Afande Hassan Lindenge na Afande Lwesya wa Jeshi la Magereza.

Friday, December 21, 2018

MKURUGENZI MKUU NHC AHIMIZA UKUSANYWAJI WA MALIMBIKIZO YA WADENI WA NHC

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea eneo la Buhare, Musoma mkoani Mara zilipojengwa nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara, kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Hazina na Uendelezaji Biashara, William Genya na Kaimu Mkuu wa Ukaguzi wa Ndani wa Shirika la Nyumba la Taifa, Abdallah Migila.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea jengo la Mukendo Commercial Complex lililopo mtaa maarufu wa Mukendo mjini Musoma mkoani Mara, kushoto kwake ni Kaimu Meneja wa NHC Mkoa wa Mara, Clifford Massau. Jengo la Mukendo la awamu ya kwanza limepangishwa lote na sasa awamu ya pili ya jengo hilo inakamilishwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea eneo la Buhare, Musoma mkoani Mara zilipojengwa nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara, kushoto kwake ni Kaimu Meneja wa NHC mkoa wa Mara Clifford Masau, Kaimu Mkurugenzi wa Ubunifu, Margareth Minja, Kaimu Mkurugenzi wa Hazina na Uendelezaji Biashara, William Genya.

Nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara zinavyoonekana.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akifuatilia maelezo ya Mhandisi anayesimamia ujenzi wa jengo la Mukendo Comercial Complex kutoka kampuni ya Kiure Engineering leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitoa maelekezo kwa Mhandisi anayesimamia ujenzi wa jengo la Mukendo Comercial Complex kutoka kampuni ya Kiure Engineering leo.




Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akisaini kitabu cha wageni katika ofisi za NHC mkoa wa Mara alipofika leo kumalizia awamu ya pili ya ziara yake kwa mikoa ya kanda ya ziwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akiwasili katika ofisi za NHC mkoa wa Mara na kukaribishwa na mmoja wa watendaji wa Shirika mkoani Mara alipofika leo kumalizia awamu ya pili ya ziara yake kwa mikoa ya kanda ya ziwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ofisi za NHC mkoa wa Mara alipofika leo kumalizia awamu ya pili ya ziara yake kwa mikoa ya kanda ya ziwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akiagana na Nyabugumba Jonathan wa ofisi za NHC mkoa wa Mara alipofika leo kumalizia awamu ya pili ya ziara yake kwa mikoa ya kanda ya ziwa


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea kushuhudia ujenzi unaoendelea wa jengo la Mukendo Comercial Complex  linalojengwa na mkandarasi kampuni ya Kiure Engineering kwa niaba ya NHC.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea kushuhudia ujenzi unaoendelea wa jengo la Mukendo Comercial Complex  linalojengwa na mkandarasi kampuni ya Kiure Engineering kwa niaba ya NHC.




Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea eneo la Buhare, Musoma mkoani Mara zilipojengwa nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara. 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea eneo la Buhare, Musoma mkoani Mara zilipojengwa nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara.





Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitembelea jengo la Utawala la Chuo Cha Kilimo la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililopo Butiama mkoani mara. Jengo hilo linajengwa na NHC kama utekelezaji wa sera ya huduma kwa jamii.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akielekeza jambo alipokuwa akitembelea eneo la Buhare, Musoma mkoani Mara zilipojengwa nyumba za gharama nafuu za Buhare mkoani Mara.
Jengo la Utawala la Chuo Cha Kilimo la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililopo Butiama mkoani mara. Jengo hilo linajengwa na NHC kama utekelezaji wa sera ya huduma kwa jamii.
Picha ya pamoja mbele ya Jengo la Utawala la Chuo Cha Kilimo la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililopo Butiama mkoani mara. Jengo hilo linajengwa na NHC kama utekelezaji wa sera ya huduma kwa jamii.
Picha ya pamoja mbele ya Jengo la Utawala la Chuo Cha Kilimo la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililopo Butiama mkoani mara. Jengo hilo linajengwa na NHC kama utekelezaji wa sera ya huduma kwa jamii.

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


Akizungumza wakati akiwa katika ofisi za NHC mkoa wa Mara, Dk Banyani alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha na kuwaeleza wafanyakazi mwelekeo mpya wa Shirika la Nyumba la Taifa kwa sasa ambao ni kujikita kwenye kuwafikia wananchi na kuwajengea nyumba za gharama nafuu.


"Tumefanya kazi kubwa sana huko nyuma kwa kujenga haya majengo makubwa ya ghorofa ili kuwafika wananchi wa viwango vyote, lakini sasa tunajikita zaidi kuwafikia wananchi wengi zaidi,älisema.


Alisisitiza wafanyakazi kila mmoja atekeleze wajibu wake ili kuliimarisha shirika liende mbele kwa kushirikiana na kuzingatia maadili ya Shirika yaliyopo kwenye mpango mkakati wa Shirika.


"Tujenge ari mpya ya kufanya kazi kwa kujiekeza na kujiandaa na mabadiliko wakati wowote, kitu pekee kisichobadilika ni mabadiliko yenyewe, lakini maisha ya binadamu na shughuli zake yanabadilika,"alisema.

Aliagiza kwamba popote panapotakiwa kujengwa nyumba basi inabidi tutafiti kwa kina na kufahamu mahitaji yao ili tuweze kujenga nyumba bora, siyo kuwakadiria wananchi. 


Pia alitaka madeni ya extenants na madeni mengine yote ya malimbikizo yafuatiliwe kwa kina ili kuweza kuwa na ufanisi katika Shirika, kwani ofisi isiyokusanya kodi ni sawa na ofisi siyofanya kazi.


Kuhusu matengenezo, alisema utaratibu mpya wa matengenezo utazingatia zaidi ufanisi na uwajibikaji na matengenezo yatazingatia vigezo kadhaa ikiwamo vyanzo vya uharibifu kama umesababishwa na mpangai au yale yaliyosababishwa na hali ya hewa au mazingira mengine.

Eneo la Buhare ni kubwa sana lenye mita za mraba za ukubwa 135,2 wakati eneo lililojengwa nyumba ni mita za mraba 10 tu.

SHIRIKA LAANZA KUFUNGUA NJIA KWENYE MAENEO YANAYOPIMWA KWAAJILI YA MAKAZI CHATO

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitoa maelekezo kwa Afisa Upimaji wa Shirika la Nyumba la Taifa, Denis Mtafya wakati alipotembelea eneo la Rubambangwe linalopimwa na Shirika la Taifa na kuanza kuuzwa kwa wananchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitoa maelekezo kwa Afisa Upimaji wa Shirika la Nyumba la Taifa, Denis Mtafya wakati alipotembelea eneo la Rubambangwe linalopimwa na Shirika la Taifa na kuanza kuuzwa kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Chato,  Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon akijadiliana jambo na ujumbe kutoka Shirika la Nyumba la Taifakuhusu utekelezaji wa miradi ya upimaji viwanja na ule wa uchoraji ramani ya ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa wa michezo wa Chato.

                                     &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk. Maulidi Banyani jana aliendelea na ziara katika miradi ya Chato apartments  na Chato affordable houses na kufanya kikao na Mkuu wa wilaya ya ChatoMhandisi Mtemi Msafiri Simeon na Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo, Eliud Leonard Mwaiteleke kuhusu miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa wilayani humo na ile iliyotekelezwa na kumueleza Mkuu wa Wilaya kuwa zoezi la kufungua barabara kwenda kwenye maeneo yanayopimwa..

Naye Mkuu wa wilaya ya Chato,  Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon aliwakaribisha ujumbe kutoka Shirika la Nyumba la Taifa na kuelezea fursa zilizopo Chato. 


Alisema kuwa Wilaya ya Chato kuna mapori ya kuvutia yakiwamo ya Burigi,  Biharamulo,  Kimisi,  Rubondo,  Rumanyika na uwanja wa ndege ambavyo vyote kwa ujumla vitaweza kuwavutia watalii wengi.


Mhandisi Msafiri alisema wao kama wilaya wanahitaji kujipanga kabla ya maendeleo kuja kuwazidi uwezo na anachokiomba ni Shirika kuendelea na upimaji wa viwanja katika eneo la Rubambangwe japo kwa awamu ya kwanza faida itakuwa ndogo. 


Dk. Banyani akizungumzia hilo alisema mradi huo ni wa kipaumbele na kwamba Shirika la Nyumba kwa sasa linajisogeza kwa wananchi kwa kuwasaidia kuwatafutia suluhu ya matatizo yao na kuwajengea nyumba bora.

Akizungumzia zoezi la kufungua barabara alisema  limeanza jana na linasimamiwa na NHC. 

Kuhusu suala la uwanja wa mpira wa Chato alisema Shirika limeandaa  concept ya uwanja huo na linaendelea kufanya tafiti sehemu mbalimbali ili kupata uwanja bora.

 Nyumba za makazi za gharama nafuu za Chato
 Nyumba za makazi za ghorofa za Chato

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akitoa maelekezo kwa Afisa Upimaji wa Shirika la Nyumba la Taifa, Denis Mtafya wakati alipotembelea eneo la Rubambangwe linalopimwa na Shirika la Taifa na kuanza kuuzwa kwa wananchi.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon baada ya kumaliza kikao Chato.
 Picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu.
  Picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chato.
 Picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chato.

 Mkuu wa wilaya ya Chato,  Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon akijadiliana jambo na ujumbe kutoka Shirika la Nyumba la Taifakuhusu utekelezaji wa miradi ya upimaji viwanja na ule wa uchoraji ramani ya ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa wa michezo wa Chato.

 Kaimu Mkurugenzi wa Hazina na Uendelezaji Biashara, William Genya akijadiliana jam Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo, Eliud Leonard Mwaiteleke jana wilayani Chato.

 
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akikagua eneo wakati alipotembelea eneo la Rubambangwe linalopimwa na Shirika la Taifa na kuanza kuuzwa kwa wananchi.
 Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Abdallah Migila akifuatilia mjadala.


 Mkurugenzi Mkuu akitafakari jambo wakat5i akikagua mradi wa upimaji viwanja wa Chato  jana.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dk Maulidi Banyani akikagua eneo wakati alipotembelea eneo la Rubambangwe wilayani Chato linalopimwa na Shirika la Taifa na kuanza kuuzwa kwa wananchi.

Mkurugenzi Mkuu akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Chato wakati Mkurugenzi Mkuu alipofika kumsalimia Mkurugenzi huyo,