Wednesday, November 29, 2017

SPIKA NDUGAI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA NHC

                                       
 Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter akimpokea Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai alipokuwa akiwasili jana kwenye makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa. Spika Ndugai alikuwa na mazungumzo na uongozi wa Shirika kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo.
 Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter akimpokea Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai alipokuwa akiwasili jana kwenye makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa. Spika Ndugai alikuwa na mazungumzo na uongozi wa Shirika kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akiwasili jana kwenye makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa. Spika Ndugai alikuwa na mazungumzo na uongozi wa Shirika kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akiwasili jana kwenye makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa. Spika Ndugai alikuwa na mazungumzo na uongozi wa Shirika kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akisalimiana na Meneja wa ofisi ya Mkurugenzi Mkuu, Muungano Saguya.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akisalimiana na Meneja wa ofisi ya Mkurugenzi Mkuu, Arden Kitomari.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akitia saini kitabu cha wageni.

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akijadili jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii, Susan Omari na Mkurugenzi wa Ubunifu Issack Peter.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai akijadili jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na Mkurugenzi wa Ubunifu wa NHC, Issack Peter.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai wakifurahia jambo na  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.

Friday, November 17, 2017

HIFADHI YA WANYAMAPORI YAKABIDHIWA GARI KUDHIBITI UJANGILI

Mwenyekiti wa HoneyGuide Foundation Olekiri Mbai akikabidhi gari aina ya Suzuki Jimmy kwa Mkuu wa Wilaya wa Monduli Iddi Hassan ikiwa ni msaada wa shirika hilo katika kusaidia hifadhi ya wanyamapori ya Randilen.

Na Woinde Shizza,Arusha.

Hifadhi ya Wanyamapori ya Randlen Community Wildlife Management, iliyoko Arusha wilayani Monduli imekabidhiwa gari aina ya Suzuki Jimmy kwa ajili ya kudhibiti vitendo vya ujangili na uharibifu wa mazingira katika hifadhi hiyo ya jamii.

Akipokea gari hilo kutoka Shirika la Honey Guide, Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Hassan alisema,  gari hilo litasaidia juhudi za kupambana na ujangili katika wilayani humo na kukuza utalii endelevu kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Akizungumza baada ya kupokea gari hilo, Hassan amesema msaada huo utasaidia kuimarisha shughuli za uhifadhi Wilayani humo, kwa kuwa kuwa hifadhi hiyo ni hifadhi pekee inayofanya vizuri katika wilaya hiyo na kunufaisha vijiji tisa vinavyozunguka hifadhi.

Alisema,msaada huo wa gari utaongeza nguvu katika mapambano dhidi ya ujangili hasa hasa katika kipindi hiki ambacho wanajipanga katika kuzuia uvunaji holela wa maliasili katika hifadhi hiyo pamoja na kuzuia ujangili

kwa upande wake, mwenyekiti wa Honey Guide Foundation Olekiri Mbai alisema, wameamua kutoa msaada huo unaogharimu kiasi cha shilingi milioni 25 ili  kusaidia shughuli za uendeshaji wa hifadhi hiyo ya jamii (WMA) katika kuunga mkono juhudi za serikali kuhakikisha kuwa uhifadhi unafanyika kwa namna ambayo unanufaisha wanajamii wa Monduli.

“Kumekua na changamoto ya Hifadhi nyingi kutokuwa na Meneja lakini hifadhi ya Randilen ni hifadhi pekee yenye meneja ambaye anasimamia shughuli zote za utawala hivyo msaada huu wa gari utamsaidia kutekeleza majukumu yake ya kila siku” Alisema Olekiri

Mwenyekiti wa Hifadhi hiyo Daniel Alais ameshukuru shirika la Honey Guide kwa kutoa msaada huo ambao utasaidia kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya ujangili na uharibifu wa mazingira ikiwa ni pamoja na kurahisisha utendaji kazi wa kila siku.

Thursday, November 16, 2017

TPDC CUP SASA RASMI SONGO SONGO


Meneja Mawasiliano TPDC akieleza umuhimu wa mashindano ya TPDC CUP katika kuboresha afya na uhusiano bora.

Bi Msellemu amefafanua kuwa, kuwepo kwa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia na Visima vya Gesi Asilia katika kijiji hicho kunaifanya TPDC kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii ya Kijiji hicho hivyo kwa kuanzishwa kwa mashindano hayo ambayo yatakuwa ya kifanyika kila mwaka ni moja ya sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa TPDC kwa Wananchi wa Songo Songo.

Aidha Meneja wa Mawasiliano ameongeza kuwa, “Mashindano haya yataambatana na zoezi la Upimaji Afya ambalo litaanza tarehe 23 hadi 25, Novemba 2017 kwa Wananchi wa Songo Songo ambalo linatarajiwa kujenga uelewa zaidi wa masula ya afya kwa wananchi wa Songo Songo na kuweza kujiepusha na maradhi mbalimbali na hivyo kujenga Jamii imara yenye Afya na Nguvu ambayo itaweza kuendesha Shughuli za Kiuchumi zitakazo jenga na kuimarisha uchumi wa Kijiji na Taifa kwa ujumla.”
Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Songo Songo na Mgeni Rasmi wa Uzinduzi wa Mashindano ya TPDC CUP wakisalimiana na Timu ya Mpira wa Miguu ya Black Rhino kabla ya kuanza kwa mechi yao dhidi ya Heroes.

Awali Meneja wa Kiwanda cha Kuchataka Gesi Asilia ndugu Kondoro Nteminyanda akiwa anamkaribisha Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa mashindano hayo alieleza kuwa uhusiano katika ya Shirika na Jamii ya Wananchi wa Songo Songo ni muhimu kwanza kwasababu wote tunategemeana katika shughuli zetu za kila siku na ili Kiwanda kiweze kifanye kazi yake kwa ufanisi kinahitaji mahusiano bora kati ya Shirika na Wananchi na hivyo shughuli kama hizi za kijamii zinazodhaminiwa na Shirika pamoja manufaa mengine lakini ni muhimu saana katika kujenga na kuendeleza ujirani mwema na ushirikiano wenye tija katika ya Kijiji na Kiwanda.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Songo Songo alieleza kuwa ni furaha ya pekee kwa Kijiji kwa Ushirikiano unaotoka TPDC haswa katika kuanishwa kwa mashindano hayo ya michezo ambayo imeleta hamasa kubwa na furaha kwa wananchi wa Songo Songo.
Mgeni Rasmi akizindua rasmi mashindano ya TPDC CUP katika Uwanja wa Mpira Songo Songo tarehe 13 Novemba, 2017.
“Ndugu zangu wachezaji wa timu zetu pamoja na mashabiki nawaomba tushiriki mashindano haya kwa kufuata Sheria za Uendeshaji wa Michezo za FIFA na Mamlaka nyingine za michezo ili tucheze kwa Amani, furaha na upendo hadi mwisho wa michuano na aliyeshindwa akubali kushindwa ili tumpe hamasa TPDC kuweza kuendelea kudhamini mashindano haya kila mwaka” alifafanua Mwenyekiti wa Kijiji.

Aidha pamoja na kulishukuru Shirika, Mwenyekiti aliomba michezo hiyo pamoja na zoezi la upimaji wa afya liwe la kudumu kama walivyopokea taarifa hapo awali.

Uzinduzi huo ulishuhudia pambano kali lililozikutanisha timu za Black Rhino na Heroes ambapo hadi mwisho wa mchezo timu Black Rhino ilifanikiwa kuitupa nje ya mashindano timu ya Heroes kwa ushindi wa gori moja kwa sifuri.

Katika Mashindano hayo Mshindi wa Kwanza wa Mpira wa Miguu atapata zawadi ya Mbuzi, Jozi moja ya Jezi na Mipira Minne, Mshindi wa Pili atapata Jozi moja ya Jezi na Mipira Miwili na Mshindi wa Tatu atapata Jozi moja ya Jezi na Mpira mmoja.Kwa upande wa Mpira wa Pete, Mshindi wa Kwanza atapata jozi moja ya Jezi na mipira miwili na Mshindi wa Pili atapata Jezi jozi moja pekee.

Mashindano yajulikanayo kama TPDC Bonanza yenye lengo la kuboresha na kuimarisha afya ya Wakazi wa Songo Songo, ushirikiano pamoja na kujenga vipaji vya michezo kwa vijana wa kike na kiume yanayodhaminiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) yamezinduliwa rasmi tarehe 13 Novemba, 2017.

Mgeni Rasmi wa Uzinduzi wa Mashindano hayo ambaye ni Meneja Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu ameeleza kuwa, “Shirika limefarijika sana kufanikiwa kuzindua Mashindano ya Michezo ya Mpira wa Miguu na Pete katika Kijiji cha Songo Songo kwa malengo ya kujenga afya bora kwa kuwa michezo ni nyenzo bora ya kuepuka magonjwa mengi yasiyoambukiza, kuibua vipaji vya michezo, kujenga na kuimarisha uhusiano bora kati ya TPDC na Wananchi.”

RAIS MSTAAFU DKT. JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAHAFALI YA 10 YA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU (DUCE) CHA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, (pichani juu), ameongoza mahafali ya kumi (10), ya  Chuo kikuu kishiriki cha Elimu (DUCEcha Chuo kikuu Dar es salaam kwenye viwanja vya chuo hicho, Chang’ombe jijini Dar es Salaam Novemba 15, 2017.
Katika mahafali hayo zaidi ya wanachuo 1,443 waliochukua mafunzo ya Shahada ya Elimu ya Jamii na Elimu, (BAED), Shahada ya Elimu ya Sayansi na Elimu, (Bsc) na Shahada ya Elimu (BED), pamoja na wahitimu waliojiendeleza (Post graduate), walitunukiwa shahada ya kwanza, ambapo mwanachuo Dadi Omary Safari, alipewa tuzo ya kuwa mwanachuo bora zaidi kitaaluma.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, akimpongeza mmoja wa wahitimu wa Shahada ya Elimu ya Jamii na Elimu, (BAED) Amisa Hassan.
Baadhi ya wahitimu katika mahafali ya 10 ya ya  Chuo kikuu kishiriki chaElimu (DUCEcha Chuo kikuu Dar es salaamwakiwa kwenye mahafali hayo
Furahaya kuhitimu na kutunukiwa shahada.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, akisoma hotuba yake.
Dkt. Kikwete, akipitia ratiba ya mahafali hayo.
Dkt. Kikwete akitangaza kuwatunuku shahada baadhi ya wanachuo hao.
Baadhi ya wanachuo wakisubiri kutunukiwa shahada zao na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete.
Dkt. Kikwete, akiteta jambo na Profesa Mukandala.
Dkt. Kikwete, akiipitia tuzo ya mwanachuo bora kitaaluma Dadi Emmanuel Safari kabla ya kumkabidhi.
Mwanachho bora kitaaluma Dadi Emmanuel Safari akiwa na tuzo yake.
 
Dkt. Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa wahitimu, Amisa Hassan, na baba mdogo wa muhitiumu huyo, Khalfan Said.

TAARIFA YA AJALI YA NDEGE YA COASTAL AVIATION ILIYOTOKEA JANA

Baadhi ya Wananchi wakishuhudia ajali katika eneo la Empakai ilipotokea ajali ya ndege ya Coastal Aviation jana mkoani Arusha,ambapo katika ajali hiyo imethibitishwa kuwa watu 11 walipoteza maisha

Tuesday, November 14, 2017

MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA AAGIZA WAFANYAKAZI NHC KUCHAPA KAZI ILI KUFIKIA MALENGO HARAKA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na wafanyakazi katika kikao chake cha kawaida ambacho hufanyika mara mbili kwa mwaka na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa ambapo pamoja na masuala mengine amewataka wafanyakazi hao kuendelea na utamaduni wa kuchapa kazi na kujenga mapenzi mema na Shirika.
Sehemu ya wafanyakazi ikifuatilia mkutano wa Mkurugenzi Mkuu pamoja na wafanyakazi ambapo mambo kadhaa yamezungumzwa.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na wafanyakazi katika kikao chake cha kawaida ambacho hufanyika mara mbili kwa mwaka na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa. 
 Sehemu ya wafanyakazi ikifuatilia mkutano wa Mkurugenzi Mkuu pamoja na wafanyakazi ambapo mambo kadhaa yamezungumzwa.
 Sehemu ya wafanyakazi ikifuatilia mkutano wa Mkurugenzi Mkuu pamoja na wafanyakazi ambapo mambo kadhaa yamezungumzwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na wafanyakazi katika kikao chake cha kawaida ambacho hufanyika mara mbili kwa mwaka na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa. 
Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu wa Shirika la Nyumba la Taifa, James Rhombo akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa .

Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifuatilia kwa karibu kikao Mkurugenzi Mkuu cha  kawaida ambacho hufanyika mara mbili kwa mwaka na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa. 

Thursday, November 09, 2017

Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wametembelea katika hifadhi ya ya Taifa ya Selous

Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wametembelea katika hifadhi ya ya Taifa ya Selous ili kutangaza utalii wa ndani kwa njia ya treni ya TAZARA. Akizungumza mwenyekiti wa umoja huo, Dkt. Liggyla Vumilia alisema kuwa wameamua kuandaa kampeni ya kutangaza utalii wa ndani kwa njia ya treni ya TAZARA hasa wa mikoa ya kusini mwa Tanzania ambao umekuwa ukisahaulika. Kampeni hiyo imeandaliwa na Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (China Alumni Association of Tanzania -CAAT) kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania - (TTB) na TAZARA. PICHA ZOTE NA KAJUNASON/MMG - SELOUS-MATAMBWE, MOROGORO.
Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wakifurahia ndani ya treni ya TAZARA wakati wakielekea ndani ya hifadhi ya Selous. 
 Ilikuwa ni furaha kila kona. 
Treni ya TAZARA ikichanja mbuga. 
 Mahojiano yakiendelea ndani ya treni.
 Moja ya pango ambao treni inapita.
 Reli ya TAZARA imenyooka.
Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wakifurahia ndani ya treni ya TAZARA wakati wakielekea ndani ya hifadhi ya Selous. 
 Makaribisho ndani ya hoteli iliyopo nje kidogo ya hifadhi ya Selous eneo la Kisaki.
 Wakipata chakula cha usiku.
 Nami mmiliki wa Kajunason Blog, Cathbert Kajuna (kulia) niliweza kuwakilisha vyema na wana-CAAT. Pembeni yangu ni Chris na Yusuph.
 Wazee wa kazi Kaijage (mbele) akiwa na Dr. Heri.
 Wana-CAAT wakipata kifungua kinywa.
 Wana-CAAT wakiwa tayari kuingia mbugani kujionea vivutio mbali mbali. Wana-CAAT wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza safari ya kuingia mbugani.
 Moja ya wanyama wanapatikana hifadhi ya Selous.
 Eneo la Matambwe gate.
 Furaha baada ya kufika eneo la geti kuu.
 Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole akitoa maelezo machache juu ya hifadhi ya Selous. PORI la akiba la Selous ni moja kati ya hifadhi zenye utajiri wa vivutio adimu vya utalii na ambavyo vinapaswa kutangazwa zaidi kwa ajili ya watalii wa ndani na wa nje. 

Selous ni pori la akiba lenye ukubwa wa kilometa za mraba 54,000 likijumuisha maeneo ya ardhi oevu, misitu ya miombo, tambarare, nyasi za kuvutia, maziwa na mito inayotiririka, vyote vikifanya vivutio vya aina yake mbali na wanyama wa aina mbalimbali. 

Pori hili la akiba la Selous lilianzishwa mwaka 1896 na Wajerumani likiwa ni pori la kwanza kutengwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori katika Bara la Afrika na la pili duniani kwa ukubwa baada ya hifadhi ya pori la Marekani ambalo linaitwa Yellowstone. Poro hili limegawanyika katika kanda 8 kiutawala. 

 Umaarufu wa Selous si katika wanyama pekee ambao ndiyo kivutio kikubwa cha utalii wa uwindaji, utafiti umebaini kuwa katika eneo la Selous kuna utajiri mkubwa wa maliasili ya mimea ambayo ikitambuliwa na kutangazwa inaweza kuwa kivutio adimu na cha kipekee cha kitalii.
 Wakisoma ramani mbali mbali inayoonyesha hifadhi hiyo.
 Moja ya ramani.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT), Dkt. Liggyla Vumilia akizungumza machache na Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole.
 Moja ya wanyama wanaopatikana katika hifadhi ya Selous.