Monday, October 02, 2017

DK.SHEIN AWAAPISHA MAJAJI WA MAHKAMA KUU YA ZANZIBAR,NA VIONGOZI WENGINE

 Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar wakipitia hati zao za viapo kabla ya kuapishwa Rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) kushika wadhifa walioteuliwa hafla ya kiapo ilifanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.
 Baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar ni miongoni mwa Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya kiapo cha Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar walioapishwa leo na Viongozi wengine kazi iliyofanya na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.
 Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar  leo, (kutoka kulia) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, Kadhi Mkuu wa Zanzibar  Sheikh Khamis Haji na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Katiba, Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora Khamis Juma Maalim.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw. Khamis Ramadhan Abdala kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bibi Aziza Iddi Suwedi kuwa  Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw. Kubingwa Mashaka Simba  kuwa  Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika  hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha  Bw. George Joseph Kazi kuwa  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika  hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, kabla alikuwa Mrajis wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya kuwaapisha rasmi leo katika hafla iliyofanyika  ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar (Picha na Ikulu).

No comments: