Tuesday, August 01, 2017

MASAUNI AWATAKA WANAFUNZI VYUO VIKUU NCHINI KUONGEZA KASI YA UBUNIFU, AFUNGUA MAONYESHO YA SAYANSI CHUO CHA ST. JOSEPH DAR


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikata utepe kuashiria kufungua Maonyesho Makubwa ya Sayansi na Teknolijia yaliyoandaliwa na wanafunzi wanaosoma fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Prakabahran Anath. Masauni baada ya kuangalia kazi za ubunifu mbalimbali uliofanywa na wanafunzi hao, aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa suti) akimsikiliza Mwanafunzi wa mwaka wanne fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, Tumaini Lutufyo (kushoto) wakati alipokuwa anatoa maelezo ya gari la kuzima moto ambalo linatumia gesi lililotengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho. Masauni alifungua Maonyesho ya Sayansi na Teknolojia chuoni hao ambapo aliangalia kazi mbalimbali za ubunifu uliofanywa na wanafunzi hao, pia aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiliendesha gari linalotumia umeme wa jua lililotengenezwa na wanafunzi wa fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam. Masauni alifungua Maonyesho ya Sayansi na Teknolojia chuoni hao ambapo aliangalia kazi mbalimbali za ubunifu uliofanywa na wanafunzi hao, pia aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo .
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, mara baada ya kufungua Maonyesho ya siku mbili ya Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Chuo hicho kwa lengo l kuonyesha ubunifu mbalimbali wa wanafunzi hao. Masauni baada ya kuangalia kazi za ubunifu mbalimbali uliofanywa na wanafunzi hao, aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, Dk. Prakabahran Anath alipokua anatoa historia ya chuo hicho kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo kufungua Maonyesho Makubwa ya Sayansi na Teknolijia yaliyoandaliwa na wanafunzi wanaosoma fani ya uhandisi chuoni hapo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

No comments: