Tuesday, August 01, 2017

MANISPAA YA KINONDONI YAKABIDHIWA SHULE YA SEKONDARI MAENDELEO


Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Benjamin Sitta akizungumza na watumishi  wa serikali na wanafunzi mapema jana katika hafla ya kupokea msaada wa shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Good Neighbour ambao ndio wadhamini wa shule hiyo, Namun Heo akizungunza na watumishi wa serikali katika hafla ya kukabidhi majengo ya shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors, jijini Dar es Salaam. 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Benjamin Sitta (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Good Neighbour,Namun Heo (kulia) wakisani hati ya makabidhiano ya shule ya sekondari ya Maendeleo iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors,mapema jana jijini Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta (wa kwanza kushoto) akiwa ameambata na watumishi wa serikali wakikagua moja ya majengo ya shule hiyo. 

Muonekano wa shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors jana jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii.

No comments: