Tuesday, May 02, 2017

MKURUGENZI MKUU WA WCF AWAHAMASISHA WAAJIRI KUJISAJILI NA MFUKO HUO, WAUNGANA NA WENZAO KUADHIMISHA MEI MOSI


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (Workers Compesation Fund – WCF), Masha Mshomba, (pichani) amewahamasisha waajiri nchini kujisajili katika mfuko huo kwani mkombozi mkubwa kwa waajiri na wafanyakazi.
Mshomba ametoa rai hiyo leo wakati wa siku ya wafanyakazi duniani ‘Mei Mosi” iliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo mgeni rasmi katika sherehe za Mei Mosi mwaka huu alikuwa rais John Pombe Magufuli. 
Mfuko wa Fidia ni mkombozi kwa waajiri na wafanyakazi nchini kwa sababu umekuja katika kipindi ambacho huko nyuma tulikuwa hatuna chombo hiki,wafanyakazi walikuwa wakipata ajali na magonjwa yanayotokana na kazi bila kupata fidia sasa mfuko umekuja mambo hayo yatakuwa historia. 

 Mshomba alisema  WCF ni faraja kwa waajiri kwani utawawezesha kujikita katika uzalishaji tu, na WCF kubaki na jukumu la kumuhudumia mfanyakazi anapoumia, au kuugua. Alsema Mshomba. Alisema pamoja na kwamba waajiri ndiyo wachangiaji wakuu,mfuko wa WCF umewaondolea mzigo wa kuhangaika na mtumishi pale anapopata ajali, au maradhi yatokanayo na kazi anazofanya. 
“Tunawasihi sana waajiri waendelee kujisajili katika mfuko wa WCF kwa haraka kabisa ili waweze kunufaika wao na wafanyakazi wao,mfanyakazi akipata ajali atapata huduma ya matibabu na kama amepata ulemavu basi atapata fidia katika malipo ya pensheni ya kila mwezi”,aliongeza Mshomba.
Katika kusherehekea sherehe za Mei Mosi mwaka 2017 mfuko wa WCF umetoa elimu kwa wafanyakazi na wananchi mbalimbali waliofika katika banda lao lakini pia wafanyakazi wa WCF wameshiriki katika maandamano ya wafanyakazi kutoka sekta mbalimbali za umma na binafsi katika viwanja vya Ushirika Moshi. Kutoka Dar es Salaam, Khalfan Said wa K-VIS BLOG anaripoti kuwa.
Wfanyakazi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), wameungana na wenzao jijini Dar es salaam kuadhimisha siku ya wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi kwa matembezi kutoka Mnazi Mmoja hadi uwanja wa Uhuru.

Kitaifa sherehe hizo zimeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli mjini Moshi ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Uchumi wa Viwanda uzingatie Haki, Maslahi na Heshima ya wafanyakazi.”

Mgeni rasmi katika sherehe za Mei Mosi jijini Dar es Salaam, alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeka, Bw. Felix Lyaviva, ambaye alipokea maandamano ya wafanyakazi na magari kadhaa kutoka taasisi za umma na binafsi yakionyesha huduma zitolewazo na taasisi hizo.
WCF ni Mfuko ulioanzishwa kwa sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi namba 20 ya mwaka 2008 na ndio Mfuko unaowajibika kutoa Mafao ya Fidia kwa Wafanyakazi walioumia, au kupatwa na maradhi yaliyoababishwa na kazi wanazozifanya lakini pia kutoa Fidia kwa wategemezi pindi Mfanyakazi anapofariki kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Wafanyakazi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (Workers Compesation Fund – WCF)  wakiwa katika maandamano
Rais John Pombe Magufuli akipokea maandamano ya wafanyakazi wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 'Mei Mosi' mwaka 2017 katika viwanja vya Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro
Wafanyakazi kutoka Mfuko wa WCF wakiwa katika banda la WCF wakati wa maadhimisho ya sherehe za Mei Mosi mwaka 2017 ambapo wananchi walipata fursa ya kupata elimu kuhusu mfuko huo
Wananchi wakiwa katika banda la WCF
Wananchi wakiwa katika banda la WCF wakipata maelezo kutoka kwa wafanyakazi wa mfuko huo
Wafanyakazi wa mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi -WCF wakibadilishana mawazo baada ya sherehe za Mei Mosi kumalizika katika viwanja vya Ushirika Moshi mkoani Moshi.Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary,katikati ni Rajabu Ruje,kulia ni Afisa Uhusiano WCF, Zaria Mmanga.
Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog
 Baadhi ya wafanyaakzi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), wakiungana na wenzao katika maandamano ya kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani ambapo kiraifa yamefanyika kwenya uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.












No comments: