Monday, April 03, 2017

UZINDUZI WA BARABARA YA MGAGADU-KIWANI KUSINI PEMBA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Kiwani na vitongoji vyake katika sherehe za uzinduzi wa barabara ya Mgagadu -Kiwani Mkoa wa Kusini Pemba uliofanyika jana,akiwa katika ziara maalum ya kikazi Kisiwani humo,(kutoka kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi (GAVU) akifuata Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano Miundombinu Mhe,Ali Abeid Karume .
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mwanajuma Majid Abdalla alipokuwa akiwasalimia Wananchi wa Kiwani na vitongoji vyake katika sherehe za uzinduzi wa barabara ya Mgagadu -Kiwani Mkoa wa Kusini Pembailiyozinduliwa na jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara maalum ya kikazi Kisiwani humo,[Picha na Ikulu.] 
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar wakiwa katika sherehe za uzinduzi wa barabara ya Mgagadu -Kiwani Mkoa wa Kusini Pemba iliyozinduliwa na jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara maalum ya kikazi Kisiwani humo.
Wananchi wa Kiwani na Vijiji jirani katika Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza nao jana katika sherehe za uzinduzi wa barabara ya Mgagadu -Kiwani,akiwa katika ziara maalum ya kikazi Kisiwani humo.

No comments: