Sunday, April 23, 2017

RC MAKALLA APOKEA MSAADA WA MIFUKO 400 YA SARUJI KUTOKA AKIBA COMMERCIAL BANK


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mh.Amos Makalla akikabidhiwa mifuko 400 ya saruji na Bi. Dora Saria ambaye ni Afisa Masoko wa Akiba Commercial Bank Jijini Mbeya.Na Mr.Pengo wa Globu ya jamii Mbeya
RC Makalla akitoa neno la shukrani mbele ya Viongozi na wafanyakazi wa Benki ya Akiba na Serikali kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mh.Amos Makalla amepokea msaada wa mifuko 400 ya saruji,kutoka kwa Benki ya AKIBA Commercial Bank Ltd ,kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa njia za Wagonjwa,yenye urefu wa mita 175 katika hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza hayo jana jijini Mbeya wakati wa kupokea msaada huo,RC Makalla aliwashukuru Wadau hao kwa kujitolea na kulishughulikia ombi lake kwa haraka na kwa uzito wa juu kabisa.

"Nawashukuru sana Wadau AKIBA Commercial Bank Ltd , kwa kulishughulikia ombi langu hili, ambalo sikutarajia kama lingechukua muda mfupi hivi,nawashukuru sana na nawaomba msichoke na  tuendelee kuijenga Mbeya yetu kwa pamoja",alisema Makalla.

Makala alisema kuwa kupitia kwa marafiki wa hospitali ya Mkoa,wanaoishi ndani na nje ya mkoa huo,kupitia harambee walioifanya hivi karibuni wamefanikiwa kukamilisha ujenzi wa mita 55 na na kuwa awamu ya pili inaendelea kwa ujenzi wa mita 175.

Mh.Makalla alisema kuwa katika awamu ya kwanza ya ujenzi huo,zilitumika fedha jumla ya shilingi milioni 600,kutokana na mahitaji kuwa makubwa ya ujenzi,ujenzi  ukasimama. kwa sababu zilikuwa zikihitajika fedha nyingine kiasi cha shilingi milioni 55,ndipo wakachukua hatua za kuomba msaada zaidi kwa wadau ambao ni AKIBA Commercial Bank Ltd .

"Kukamilika kwa ujenzi huu kutaondoa tatizo la wagonjwa kupelekwa au kwenda wodini kwa taabu, kwani wakati wa mvua tatizo linakuwa kubwa ",alisema Mh Makalla.

Kwa upande wa Akiba Commercial Bank kupitia kwa Afisa Masoko na Uendeshaji Bi Dora Saria amesema waliguswa sana baada ya kuombwa na Mkuu wa Mkoa kutokana na wananchi kupata shida hasa wagonjwa kwenda wodini au kupeleka maiti kwenye chumba cha kuhifadhia maiti

Hivyo wao kama taasisi ya Benki waliguswa na jambo hilo,na wakachukua hatua ya kuchangia shilingi milioni 5 sawa na Mifuko 400 ya saruji na kuahidi kutoa Mafunzo na mikopo kwa wajasiriamali 

Aidha Akiba wamevutiwa na jitihada za Mkuu wa Mkoa kuliweka jiji safi hivyo watatoa Vifaa vya usafi na kushiriki kufanya usafi mwisho wa mwezi huu.

No comments: