Friday, March 24, 2017

Waziri Mwakyembe Apokelewa na Wafanyakazi Wa Wizara Yake


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akipokelewa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Annastazia James Wambura katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO mala baada ya kutoka kula kiapo leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akipokea shada la maua kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Wizara hiyo Bi. Flora Mwnyenyembegu wakati wa mapokezi ya Waziri huyo yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Annastazia James Wambura(wapili kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Nuru Khalfan Milao wakati wa mapokezi ya Waziri huyo yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari – MAELEZO Bibi. Zamaradi Kawawa wakati wa mapokezi ya Waziri huyo yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Yusuph Omary wakati wa mapokezi ya Waziri huyo yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiweka saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kupokelewa na watendaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Taasisi zake, mapokezi yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Annastazia James Wambura.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa OElisante Ole Gabriel akimtambulishaKatibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (kushoto)kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati), wakati wa mapokezi ya Waziri huyo yaliyofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam. 

Picha zote na Frank Shija

No comments: