Sunday, March 19, 2017

Naibu Waziri wa Ardhi Dk. Angelina Mabula alifanya ziara kwenye mradi wa Nyumba wa NHC (Sarafari City) jijini Arusha.

sa1
 Baadhi ya Watumishi wa shirika la nyumba mkoa wa Arusha wakimsikiliza Naibu waziri Mabula alipotembelea na kukagua nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba hapo (PICHA NA MUUNGANO SAGUYA-NHC)
sa2
 Baadhi ya Watumishi wa shirika la nyumba mkoa wa Arusha wakimsikiliza Naibu waziri Mabula alipotembelea na kukagua nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba hapo jana.
sa3
 Meneja wa shirika la nyumba (NHC) mkoa wa Arusha James Kisarika akitoa maelezo ya ramani ya mradi wa nyumba na mji wa kisasa wa Safari city unaojengwa na shirika hilo katika eneo la Mateves jijini Arusha .
sa4
Meneja wa shirika la nyumba mkoa wa Arusha James Kisarika akimwonyesha Naibu waziri Mabula, eneo linalotarajiwa kuwekeza majengo kwa ajili ya viwanda na biashara katika mradi wa nyumba wa Safari City.
sa5
Naibu Waziri Angelina Mabula na Viongozi mbalimbali wa shirika la nyumba na sekta ya ardhi wakipita kukagua nyumba za mradi wa mji wa kisasa wa safari city jijini Arusha, alipotembelea mradi huo hapo jana.
sa6
 Naibu Waziri Angelina Mabula akipewa maelezo na Meneja wa NHC mkoa wa Arusha James Kisarika alipokagua jengo linalotarajiwa kuhamishiwa ofisi ya ardhi kanda ya kaskazini inayohamia Arusha kutoka Moshi.
sa7
 Naibu waziri Mabula akikagua kumbukumbu mbalimbali katika masijala ya Ardhi ya halmashauri ya jiji la Arusha.
sa8
 Naibu Waziri Mabula akiongea na Watumishi wa sekta ya Ardhi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha,kulia kwake ni Kaimu katibu Tawala Mkoa na Mkurugenzi wa jiji..
sa9
 Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi Angelina Mabula akitoa maelekezo ya uboreshaji wa miradi inayotekelezwa na shirika la nyumba nchini, alipotembelea mradi wa nyumba wa Safari City Arusha.
sa10
 Naibu waziri wa Ardhi, nyumba, na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi walioambatana naye kukagua mradi wa nyumba safari City jijini Arusha jana.
sa11
Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, na mendeleo ya makazi Angelina Mabula akikagua mifumo ya ulipaji kodi ya ardhi alipotembelea halmashauri ya jiji Arusha, kulia kwake ni mkurugenzi wa jiji Athuman Kihamia .
sa13
 Sehehemu ya Nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la nyumba nchini (NHC) katika mji wa kisasa wa safari city, jijini Arusha, nyumba hizo zinatarajiwa kuuzwa zitakapokamilika.

No comments: