Monday, January 16, 2017

MASHINDANO YA NAGE MAPINDUZI CUP YAFIKIA TAMATI, NAIBU WAZIRI NGONYANI, MASAUNI WAMWAGA ZAWADI KWA WASHINDI

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani akiwasalimia wachezaji wa Karakana City wakati akikagua timu za mchezo wa Nage zilizoingia Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017. Aliyevaa kofia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, ambaye ndiyo mwandaaji wa Mashindano hayo. Ngonyani aliyafunga Mashindano hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani akizungumza na mamia ya wananchi waliouhudhuria katika Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, ambaye ndiyo mwandaaji wa Mashindano hayo. Ngonyani aliyafunga Mashindano hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala. Katika mashindano hayo, timu ya Six Centre iliibuka mshindi dhidi ya timu ya Karakana City zote za mjini Unguja. Picha na Felix Mwagara.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani (wapili kulia) kuja kufunga Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Katika hotuba yake Masauni ambaye ndiyo aliyeandaa msahindano hayo alisema, mchezo huo utazidi kuthaminiwa ili kuwaweka vijana pamoja. Picha na Felix Mwagara.
Mchezaji wa timu ya Six Centre ya Mwera ambayo imepata ushindi, akikwepa mpira katika mchezo wa Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017, kati ya timu hiyo na Karakana City ya Chumbuni, katika viwanja vya Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.
Msanii wa kizazi kipya, Kheri Sameer Rajab (Mr. Blue), akitoa burudani huku akishangiliwa na Waheshimiwa Wabunge pamoja na Wawakilishi wakati wa Fainali za Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. , Watatu kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akifuatiwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala. Picha na Felix Mwagara.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiwa katika picha ya pozi na Msanii wa nyimbo za Singeli, Manfongo kabla ya msanii huyo kupanda jukwaa kutoa burudani katika
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, (watatu kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na wasanii maarufu wa kizazi kipya kutoka Tanzania Bara na Visiwani kabla ya Wasanii hao kupanda jukwaani kutoa burudani katika Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yaliandaliwa na Mhandisi Masauni ili kukuza vipaji vya vijana. Picha zote na Felix Mwagara.

No comments: