Thursday, August 04, 2016

VIONGOZI WA DINI WAOMBEA UWANJA WA NDEGE WA TERMINAL III UNAOENDELEA KUJENGWA JIJINI DAR LEO.

Katibu wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam na kiongozi wa Kanisa la Anglikana, Mchungaji,John Solom(aliyeshika kipaza Sauti) akisali kuombea uwanja wa ndege wa Terminal III unaoendelea kujengwa leo jijini Dar es Salaam uliopo katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Mradi wa Mamlaka ya Anga Tanzania (TAA), Mhandisi, Mohamed Milanga akitoa maelekezo kwa viongozi mbalimbali wa dini jijini Dar es Salaam leo walipotembelea na kuombea uwanja mpya wa ndege unaoendelea kujengwa wa Teminal III uliopo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere. 
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum akiomba dua  kuombea uwanja wa ndege wa Terminal III unaoendelea kujengwa leo jijini Dar es Salaam uliopo katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Wengine ni Viongozi mbalimbali wa Dini.
  Katibu Mkuu wa Kampuni wa Mamlaka ya Anga Tanzania, Jaji Ramdhan Maleta(Mwenye tai Nyekundu) akitoa neno la Shukrani mara baada ya kumaliza ziara ya viongozi mbalimbali wa dini waliotembelea katika uwanja wa ndege unaoendelea kugengwa wa Terminal III jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Yasir Adam, Globu ya Jamii.

No comments: