Sunday, August 07, 2016

UVCCM ARUSHA YATOA MIFUKO 100 YA SIMENTI KWA AJILI YA BWENI LA SHULE YA NANJA LILILOTEKETEA KWA MOTO


Viongozi wa UVCCM mkoa wa Arusha wakiwa wanatembelea shule ya Sekondari ya Nanja ilioungua na moto Julai 2 mwaka huu

mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha Sabaya Lengai wa pili kushoto akiwa anaangalia bweni la shule ya Nanja lililoungua na moto

Mwenyekiti wa UVCCM Arusha akiwa na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Nanja ilioungua na moto hivi karibuni wakati alipoenda kutembelea shule hiyo na kutoa mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa bweni la shule hiyo lililoungua na moto





Na Woinde Shizza,Arusha

Umoja wa vijana Wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Arusha wamehaidi mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari Nanja iliopo wilayani Monduli mkoani Arusha iliyounguliwa bweni na moto mapema july 2 mwaka huu

Akiongea na wanafunzi wa shule hiyo mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha Sabaya Lengai alisema kuwa wao kama vijana wa ccm mkoani hapa wameguswa sana na tukio hilo ndio maana wakaamua kujikusanya na kwenda kutembelea shule hiyo pamoja na kuwapa mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa bweni ambalo limeungua.

Alisema kuwa wao kama vijana wanamoyo na wananguvu hivyo wako tayari kuwasaidia wadogo zao ambao wapo mashuleni na ndio maana wameamua kutoa mifuko hiyo.

"unajua atuna ela nyingi lakini tumeamua kuwapa msaada hawa wadogo zetu ili wasome kwa raha na wasiwe na mawazo kabisa kuhusia na tatizolililo wakuta na ndio maana wameamua kuwapa msaada huo"alisema Sabaya

Alisema kuwa mchawi hatoki mbali ivyo ni wajibu wa kila mwanafunzi kufanya uchunguzi na iwapo ata jua nani alisababisha bweni hilo likaungua watoe taarifa katika ngazi usika.

Aliwatoa hofu wanafunzi hao kwa kuwasihi wasiwe na wasiwasi wa kuishi shuleni hapo kwani serekali ya chama cha mapinduzi chini ya Rais wake John Magufuli ipo makini katika swala zima la ulinzi na imeimarisha ulinzi shuleni hapo hivyo wasome wakiwa na amani kabisa wakijua kuwa kunawatu wanawalainda.

Kwa upande wake katibu wa UVCCM wilaya ya Arusha Ezekiel Molel aliwasihi wanafunzi hao kuzingatia masomo kwani amna urithi wowote wanaoweza kupewa na walimu wao zaidi ya elimu

Aliongeza kuha haya yanayotokea ni matatizo ya kawaida ivyo wasiyaweke akilini bali waangalie swala la kusoma na fate sana elimu maana bila elimu amna kitu chochote ambacho wanawezakukipata katika miaka hii .

"serekali ya sasa hivi aina mambo ya kona kona hivyo wadogo zangu naomba niwasihi msome sana mzingatie elimu maana bila elimu hamna kitu chochote kinachoweza kufanyika kwanielimu ni kila kitu kwa kipindi hata mnavyotuona sisi hapa sisi wenyewe tumesoma na tunakazi na ndio maana leo hii tumeweza kuja kuwapa pole na kuchangia hiyo mifuko 100 tungekuwa atuna elimu hata kuja hapa au kufanya hizi kazi tusingeweza "alisema Molell

Aliwaambia kuwa ata vitabu vya dini vimeaandika waishikilie sana elimu na wasiiacha iende zake hivyo ni wajibu wao kuweka akili zao katika swala zima la elimu na sio kungine ,aliongeza kuwa sasa ivi kuna gonjwa hatari la ukimwi hivyo ni wajibu wao wanafunzi ambao ni taifa la kesho kuhakikisha wanaepuka vishawishi mbalimbali ambavyo vinaweza jitokeza

No comments: