Tuesday, August 23, 2016

UFUNGUZI WA MAFUNZO KUHUSU MWONGOZO WA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UMMA KWA MIKOA YA KANDA YA ZIWA


Mgeni Rasmi Bw. Maduka Paul Kessy, Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uzalishaji, Tume ya Mipango (aliyesimama) akitoa hotuba kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Rasilimali za Umma kwa washiriki kutoka mikoa ya Mwanza, Mara, Geita and Simiyu. Wengine ni Bi. Lorah Madete, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango (kushoto) na Bw. John Mduma, Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (kulia).
 Muwezeshaji Dr. Kenneth Mdadila, Mhadhiri, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akishusha nondo kwa washiriki wa mafunzo hayo.
 Washiriki wa Mafunzo wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayofanyika Jijini Mwanza katika Ukumbi wa Chuo cha Ufundi Stadi (Veta).
 Washiriki wakisikiliza na kufuatilia kwa makini mafunzo waliyokua wakipata kutoka kwa muwezeshaji.
Washiriki wa mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Rasilimali za Umma kutoka mikoa ya Mwanza, Mara, Geita and Simiyu pamoja na wawezeshaji wa mafunzo wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.

Picha zote Na: Thomas Nyindo-Tume ya Mipango

No comments: