Friday, August 19, 2016

TIC YATEMBELEA NA KUKAGUA SHUGHULI ZA UWEKEZAJI WA MAKAMPUNI NCHINI

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Cliford Tandari akisikiliza na kuandika maelezo ya Pastory Mroso Meneja Mkuu wa Mlimani City Group wakati alipotembelea mradi mpya wa ujenzi wa kumbi mpya za mikutano na kujionea maendeleo ya ujenzi huo, Mkurugenzi huyo amefanya ziara hiyo ili kuona maendeleo na shughuli za uwekezaji wa kampuni hiyo nchini hapa nchini ili kutambua changamoto na mafanikio yaliyopo katika uwekezaji wa kampuni hiyo hapa nchini, waliosimama nyima kutoka kushoto ni Pendo Gondwe Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC , Phina Lyimo Meneja Uhamasishaji na Uwekezaji TIC na Veronica Mrema Afisa Uhamasishaji na Uwekezaji TIC.
Kamimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Cliford Tandari akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa kituo hicho kutoka kulia ni Phina Lyimo Meneja Uhamasishaji na Uwekezaji TIC na Veronica Mrema Afisa Uhamasishaji na Uwekezaji TIC na Pendo Gondwe Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC wakati Kaimu Mkurugenzi huyo alipotembelea ujenzi wa kumbi mpya za Mlimani City.
Kamimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Cliford Tandari akiteta jambo na Pendo Gondwe Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC leo alipotembelea na kukagua ujenzi kumbi mpya za Mlimani City.Kamimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Cliford Tandari
Kamimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Cliford Tandari akionyeshwa picha ya kumbi mpya za Mlimani City zinazoendelea kujengwa hazipo pichani na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mlimani City Group Pastory Mroso wakati alipotembelea mradi huo ili kuona maendeleo ya uwekezaji wa kampuni hiyo nchini.
Meneja Bidhaa Mwandamizi wa Kampuni ya Super Doll .inayotengeneza matela ya maroli iliyo chini ya kampuni mama ya Super Star Group Bw. Ibrahim Juma akiwaelezea wahariri wa vyombo vya habari na waandishi wakati walipoitembelea kampuni hiyo ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ili kuona tija na changamoto za uwekezaji wa kampuni hiyo hapa nchini, Ziara hiyo iliandaliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC.
Meneja Bidhaa Mwandamizi wa Kampuni ya Super Doll .inayotengeneza matela ya maroli iliyo chini ya kampuni mama ya Super Star Group Bw. Ibrahim Juma akifafanua jambo kwa wahariri wa vyombo vya habari na waandishi wakati walipoitembelea kampuni hiyo ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ili kuona tija na changamoto za uwekezaji wa kampuni hiyo hapa nchini, Ziara hiyo iliandaliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC.

No comments: