Friday, August 19, 2016

TAMWA YAWAKUTANISHA WANAHABARI KANDA YA ZIWA KUJADILI MAFANIKIO NA CHANGAMOTO KABLA NA BAADA YA UCHAGUZI MKUU.


Chama cha Wanahabari Wanawake nchini, TAMWA, kimewakutanisha wanahabari kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa, kujadili namna mafunzo yaliyotolewa na chama hicho kwa wanahabari hao wakati wa kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, kwa kuangazia usawa wa kijinsia kati ya Wanawake na Wanaume katika mchakato wa uchaguzi huo.

Pichani ni wanahabari hao wakiwa kwenye semina ya siku mbili kuanzia leo, inayofafanyika Jijini Mwanza, ambapo imelenga kujadili namna mafunzo yaliyotolewa mwaka jana na TAMWA kwa kushirikiana na taasisi ya INTERNEWS yalivyosaidia katika suala la usawa wa kijinsia kabla na baada ya uchaguzi mkuu pamoja na changamoto zilizojitokeza.

Na George Binagi-GB Pazzo

Mkufunzi wa semina hiyo, Deodetus Balile, ambaye pia ni Mhariri gazeti la Jamuhuri.
Semina kwa Wanahabari Kanda ya Ziwa
Godfrida Jola (kulia) akiteta jambo na Edson Sosten (kushoto), wote ni Maafisa Miradi TAMWA.
Baadhi ya Wanahabari Kanda ya Ziwa, wanaoshiriki Semina ya TAMWA Jijini Mwanza
Wanasemina

Tazama Hapa Semina ya Mwaka Jana

No comments: