Friday, August 26, 2016

DC WILAYA YA LONGIDO AONYA WASIMIAMIZI WA MITIHANI SHULE ZA MSINGI KUWA MAKINI

index

NA MWANDISHI WETU
MKUU wa Wilaya ya Longido, Daniel Chongolo, amewaasa wasimamizi wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kutofanya kazi hiyo kwa mazoea  ili kutoruhusu mianya itakayowafanya wanafunzi wasiokuwa na uelewa kufaulu mtihani huo.
Alisema  kumekuwa na baadhi ya wanafunzi wasiojuka kusoma na kuandika kufaulu mithani hiyo kitendo kinachotia mashaka kwa wasimamizi hao kushindwa kunyakazi hiyo kwa makini.
Chongolo aliyasema hayo jana, wakati akizindua semina ya mafunzo kwa wasimamizi hao wilayani Londogo ambapo alisema usimamizi hafifu wa mitihani umesababisha kuwepo kwa watumishi wasiokuwa na uwezo kitaaluma.
Alisema iwapo ikibainika kufaulu kwa wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika mtuhumiwa wa kwanza kwenye uzembe huo atakuwa msimamizi wa mtihani.
“Nawatahadharisha kwamba mnaweza mkarubuniwa kuwawezesha wanafunzi wasiokuwa na sifa wafaulu mtihani huo, kufanya hivyo ni kukiuka kanuni za usimamizi na uendeshaji wa mtihani,” alisisitiza.
Hivyo aliwataka wasimamizi hao kuwa makini katika kufanyakazi hiyo na kama kuna jambo lolote ambalo hawajalielewa kuhusu kazi hiyo ni vyema wakauliza ili kupewa majibu.
Alibainisha kuwa, serikali imezingatia uwezo wa kitaaluma, uadilifu na uaminifu hivyo  wasimamizi hao kupewa jukumu la kusimamia mitihani hiyo muhimu ya kitaifa.
Aliongeza kuwa mitihani huo ni muhimu ili kuliwezesha taifa kupima kiwango cha elimu kilichpo nchini.

No comments: